Huduma za Kifedha
Hawala ya Fedha Ndani ya Nchi (IMO)
Huu ni uhamishaji wa fedha wa papo kwa papo ndani ya Afrika Mashariki, yaani Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Zimbabwe na Tanzania.
Fedha Taslimu Posta
Inatumia teknolojia ya kisasa (Utumaji wa Kimtandao) kwa ajili ya kutuma na kupokea fedha kwa gharama nafuu ndani ya nchi. "Ni fedha za papo kwa papo"
Uhamishaji wa Fedha Toka Akaunti Moja kwenda Nyingine
Inashughulika na kuchukua na kulipa kwa wateja kwa niaba ya makampuni, mabenki na mashirika ambayo yana mawasiliano na shirika.
Ubadilishaji wa Fedha za Kigeni Posta
Huduma hii inatoa huduma za kubadilisha fedha kwa kiwango bora zaidi cha bei. Kwa sasa, huduma zinapatikana Ofisi Kuu ya Posta (GPO) Dar es Salaam.
Huduma za Wakala
Huduma hizi zinatolewa kupitia mtandao wa posta kwa kuzingatia makubaliano kati ya shirika na mteja mfano: Western Union, Benki ya Posta, Bima, n.k.
Sehemu za Kupata Huduma za Intaneti
Wateja wanaweza kupata intaneti na huduma za uhazili kwa viwango nafuu vya bei katika ofisi zote za posta makao makuu, wilaya na baadhi ya vituo vya biashara.
Duka la Posta
Hivi ni vituo vya Posta ndani ya mtandao wa posta ambapo wateja wanaweza kununua vitu mbalimbali kwa gharama nafuu.