JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SHIRIKA LA POSTA TANZANIA

Habari

MAADHIMISHO YA SIKU YA POSTA DUNIANI 2


 

MAADHIMISHO YA SIKU YA POSTA DUNIANI

81CC6925 A25E 41F5 B0B2 D1636D6EC67B

 Na mwandishi wetu,Dar es salaam

*Uzinduzi wa Stempu ya Pamoja na nchi
ya Oman
*Uzinduzi wa Stampy ya Tanzabia
inayohamasisha utalii wa ndani (Royal
Tour)

Tanzania kupitia Shirika la Posta kwa kushirikiana na Posta Oman imezindua Stempu ya Pamoja yenye lengo la kutunza na kuendeleza uhusiano wa kihistoria ulipo baina ya nchi hizi mbili. Pia Tanzania imezindua Stempu maalum yenye lengo la kuhamasisha utalii wa ndani (Royal Tour)

Stempu hizo zimezinduliwa rasmi na Mheshimiwa Nape Nnauye, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Posta Duniani yaliyofanyika Tarehe 9 Oktoba,2022 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na Naibu Balozi wa Oman Bwana Rashid Al-Manji aliyeongozana na Mtendaji Mkuu wa Posta ya Oman na Asyad Group Nasser Al Sharji pamoja na viongozi wengine kutoka Posta Oman na baadhi ya Viongozi kutoka nchini Tanzania.

Aidha, Stempu ya Pamoja na nchi ya Oman imetumia mchoro wa jengo la Maajabu maarufu kama "House of Wonders" lililopo Stone Town, Zanzibar, lengo ikiwa ni kutunza historia ya jengo hili ambalo lina mchango mkubwa kihistoria kati ya nchi hizi mbili.

Vilevile Stempu ya nchini Tanzania imetumia michoro ya wanyama wakubwa nchini yaani “Big Five” ikiwemo Simba, Tembo, Chui, Nyati na Faru, lengo ikiwa kuhamasisha utalii.

Ushirikiano wa Shirika la Posta Tanzania na Posta ya Oman ni muendelezo wa ushirikiano unaoendelea kutekelezwa na viongozi wa nchi hizi mbili.

Ikumbukwe kuwa Juni, 2022, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alitembelea nchi ya Oman pamoja na kuona namna ambavyo Posta ya nchini humo inafanya shughuli zake katika kuhudumia wananchi.

Ushirikiano huu ni endelevu na wenye tija katika kuhakikisha wananchi wananufaika na ushirikiano uliyopo, hususani katika huduma mbalimbali zinazotelewa katika nchi hizi hasa katika Sekta ya Posta.

Picha za matukio zaidi

CB0D3480 D45D 4EA3 AF09 BA4424BB0D4D 

 A5C0539A F32D 4524 ADF3 4B4B3C018D6F

 CB6B3110 F2A0 4E20 866D 1770B0EC07D1

 D883C1E3 ABDE 43AA A8B6 2ACF91B30FC0

 DADA1E50 1CA8 4AC5 ADC3 C0B9215851CB

 6E66D02D 166C 4D05 969D E5DB694A4737

 361BAE38 EA02 4816 9943 0704C2BD17A3

 95EF087B 505A 4940 BE45 99A2FAA89644

 78C0311F EB1C 4595 849C 69EEBB7DD5FC

 48EB6CDC 6913 4CED 90D9 CD69BE717090

 6A7824FE C3DE 4161 B8B5 5454A704DC8C

 785C6CD3 6C3E 4047 80A7 C2A7E74C5E5A

2826F7A9 4C2A 412A 990A 7EDF75FC4E40

 9CA7CCC7 1911 4E8F AE48 D3B36EEB97B0

 8291146C A31C 4927 991D 5C626DC07CA9

 E12B4AE8 D109 4BAA 94DE 2F35D6A7EC1C

 A684613B FF47 4E6A AD88 2D3EABAEC5EC

 0C0A99A3 0252 4B6E B6A1 B24E763F3CE0

 

Rudi Juu

© SHIRIKA LA POSTA TANZANIA 2023